Faith in God is not an Option

Blogger WidgetsJesus Loves You

Monday, 25 November 2013

Ni nini mafundisho ya Yesu juu ya Mali?

Mafundisho ya Yesu juu ya fedha yanaonyesha yeye ndo mtoaji wa mali zote tulizonazo kuanzia kidogo mpaka kikubwa, je si vyema kushukuru kwa hiki kidogo tulichonacho?, Kuna njia nyingi tunazoweza kurudisha shukrani zetu kwake moja wapo ni kujitolea mali alizotupatia ili zifanye kazi yake aliyotuachia ya kuokoa roho za watu kwa kuwafundika ukweli kuusu wokovu. Ukifanikisha roho moja kufahamu ukweli basi utakuwa umejiwekea azina kubwa sana mbinguni." Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba, 20 bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi, 21 kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako"(Mathayo 6:19-21).

Tujifunze kutoa kwa moyo wenye furaha maana Yesu anatuambia tuwe macho sana na choyo na wala wingi wa mali ulizonazo au kuzishikirai haziwezi kukupa uzima hata wa dakika moja, sasa ni vyema kutambua ya kwamba inatupasa kumtolea Mungu katika kazi yake. "Kisha akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo. '( Luka 12:15).

Kama tutaweka akili zetu katika mali tulizonazo na kusahau kabisa kwa nini Mungu ametupatia mali hizo  ni sawa na kutumikia mali kuliko Mungu, Sasa ni wajibu wa kila mmoja wetu kutumia mibaraka aliyopewa katika kuitangaza kazi ya Mungu. Andiko linasema"  Hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana, ama atamchukia huyu na kumpenda huyu, ama atashikamana na huyu na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali. 14 Basi Mafarisayo, ambao wenyewe ni wapenda fedha, waliyasikia hayo yote, wakamdhihaki. 15 Akawaambia, Ninyi ndinyi mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu awajua mioyo yenu; kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu"( Luka 16 : 13-15). Basi liwe fundisho kwetu pia

Yesu alitufundisha kutokuwa na wasiwasi kwa kuwaza tutaishi vipi, kuna mifano mingi sana katika biblia inayoonyesha mibaraka ya kutoa kwa Moyo. Kwa kuwa yeye ndio mtoaji anatuambia "  Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa."(Mathayo 6:31-33 ). Inatupasa kusumbukia wokovu zaidi ya mali, Yesu anatuambia tusisumbukie maisha yenu kwamba tutakula nini au kuvaa nini Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.  Haiishi hapo tu anasema “Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana ghala wala uchaga, na Mungu huwalisha”. Je sisi si Bora ninyi kuliko ndege? Tuishi kwa Imani na kutumia mali zetu katika kazi ya Mungu maana ni azina yetu mbinguni kuliko kutumia kwa anasa za dunia hii.
Mungu awabariki tunapoendelea kujitolea kwa ajili ya mkutano wetu mkuu tuliouandaa kama kundi kwa ajili ya kutangaza wokovu wa Mungu, Mda umekwisha si mbali tutafika ngambo ya mto.

*******Mahubiri yataanza 1/12/2013. kwa WIKI MBILI, .eneo la NZASA -Mbagala********
NAMBA ZA MICHANGO NI: TIGO PESA. :::0712 341 748. M-PESA:: 0754 950 444. AIRTEL-MONEY :: 0782 950 444. TUJITOE kwa MAOMBI YASIYO KOMA  na MALI ZETU, kufanya kazi TULIO ITIWA KANISANI, MUDA wa Kupeleka INJILI. kwa AMANI, unakaribiakwisha. 

Koyison J

Sunday, 17 November 2013

Namna ya Kushinda hisia ya Hatia.

Kila mmoja katika maisha haya kuna dhambi amewahi fanya, ambayo angependa ibaki kuwa siri, maana ni mbaya!! Dhambi au jambo ambalo mara nyingi shetani humletea mawazoni na kumwambia “wewe hufai, si unakumbuka ulifanya hivi na vile”. Kwa hiyo kila Ombi lako linaposhindwa kujibiwa au kila unapopitia changamoto za maisha, wazo linapandikizwa kichwani kwamba Mungu hakunisamehe ile dhambi , Au ananipa adhabu kwa kile nilichokifanya, na mtu anakosa raha, au anapiga magoti tena kumuomba Mungu msamaha kwa jambo ambalo alishaliombea msamaha ila ameingiwa na wasiwasi kwamba bado hajasamehewa.
Dhambi hizo zaweza kuwa ni kutoa Mimba, Kula zaka, Kumtukana mzazi wako, Kumwacha mchumba wako akiwa bado anakupenda, n.k. Kwa hiyo kama mtu aliwahi toa mimba, na alipoolewa au kuoa akawa hapati mtoto, basi moja kwa moja hudhani Mungu hajamsamehe na ndio anamwadhibu sasa. Anasahau kwamba Sara na Ibrahimu walikuwa hawajawahi kutoa mimba lakini walikuwa hawapati watoto, mpaka Mungu alipowafanyia muujiza uzeeni. Na mifano mingine ya aina hiyo.

Hatia huleta wasiwasi na magonjwa na hata msongo mbaya wa Mawazo. Hatia pia hufanya imani yako kwa Mungu iingiwe na mashaka. Hatia ni mbaya sana!

NAMNA YA KUSHINDA HATIA

Mpe Yesu hisia yako ya hatia kwa njia ya maombi.

Mwambie Yesu kwamba unaomba akusamehe dhambi hiyo uliyoitenda, ijutie na Muombe akupe msamaha.

“This feeling of guiltiness must be laid at the foot of the cross of Calvary. The sense of sinfulness has poisoned the springs of life and true happiness. Now Jesus says, Lay it all on Me; I will take your sin, I will give you peace. Destroy no longer your self-respect, for I have bought you with the price of My own blood. You are Mine; your weakened will I will strengthen; your remorse for sin I will remove”. {2MCP 451.2}

Siku ikitokea kwamba Wazo la hatia linakurudia, Piga magoti mwambie Yesu ninajua umeshanisamehe, mimi ni mtoto wako, hukumbuki lolote nililolifanya maana wewe unasamehe na kusahau. Na shetani ushindwe katika jina la Yesu maana huna mamlaka ya kunihukumu maana niko ndani ya Yesu. Ukiomba kwa namna hiyo (Usikariri maneno haya, tumia ya kwako binafsi), utaona hisia hizo za hatia zinaisha kwa jina la Yesu lakini inakupasa uombe kwa imani.

“Satan seeks to draw our minds away from the mighty Helper, to lead us to ponder over our degeneration of soul. But though Jesus sees the guilt of the past, He speaks pardon; and we should not dishonor Him by doubting His love”.--Lt 2, 1914. (Testimonie to Ministers 518.) {Mind,Character and Personality, Vol 2 page 451.4}

Mungu akubariki, unapoamua kuikataa hisia hii mbaya ya hatia na kupeleka dhambi zako kwa Yesu ili usamehewe na kuamini kuwa Umeshasamehewa milele na Mungu hakumbuki tena. Mungu akubariki sana.


Kanyika Lusato

Wednesday, 13 November 2013

Masimulizi Yanayomhusu Yesu Yaliandikwa Lini?

Mtume Yohana aliandika hivi kuhusu mambo aliyoripoti kuhusu maisha ya Yesu: “Yeye ambaye ameona hilo ametoa ushahidi, nao ushahidi wake ni wa kweli, na mtu huyo anajua kwamba yeye husema mambo ya kweli, ili ninyi pia mweze kuamini.”—Yohana 19:35. Sababu moja ya kuamini masimulizi ya Injili yaliyoandikwa na Mathayo, Marko, Luka, na Yohana ni kwamba waliandika wakati watu wengi waliojionea matukio hayo bado walikuwa hai. Kulingana na chanzo kimoja cha habari, Injili ya Mathayo iliandikwa katika mwaka wa nane baada ya kifo cha Yesu, yaani, karibu mwaka wa 41 W.K. Wasomi wengi wanasema Injili hiyo iliandikwa baadaye, lakini wote wanakubali kwamba vitabu vyote vya Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki viliandikwa katika karne ya kwanza W.K. Watu waliomwona Yesu akiwa hai duniani, waliojionea akifa, na akifufuliwa na wangethibitisha masimulizi ya Injili. Pia, wangefunua mambo yoyote ambayo hayakuandikwa vizuri, ikiwa yalikuwapo. Profesa F. F. Bruce anasema hivi: “Mojawapo ya mambo yenye nguvu katika mahubiri ya awali ya mitume ni uvutio wenye uhakika kwa maarifa ya wasikiaji; si kwamba walisema tu, ‘Sisi ni mashahidi wa mambo haya,’ bali pia, ‘Kama mjuavyo nyinyi wenyewe’ (Matendo 2:22).”

Dk Syaga James

Thursday, 7 November 2013

Shetani ni Nani...?


Imani ya watu kuhusu shetani huwa tofauti kutoka kutojua hadi upotovu kutokana kwa kijana mdogo mwekundu aliye na pembe anaketi juu ya mabega yako akikusii utende dhambi, ni elezolimetolewa likitambulisha jinsi dhambi simehuishwa. Bibilia ingawa inatupa picha kamili vile Shetani alivyo na vile anavyo shawishi maisha yetu. Lakini kwa uchache, Bibilia inamfafanua Shetani kama malaika aliyeanguka kutoka kwa nafasi yake mbinguni kwa sababu ya dhambi na sasa anampinga Mungu, akifanya juhudi zake ili ageuze mapenzi ya Mungu.

Shetani aliumbwa malaika mtakatifu. Isaya 14:12 inampa Shetani jina kabla aanguke kuwa nyota ya alfajiri. Ezekieli 28:12-14 inamwelezea Shetani kuwa, aliumbwa awe kerubi, kawaida mlaika mkuu. Aligeuka na kuwa mkali kwa ajili ya urembo wake na cheo chake na akaamua kuwa aketi kwenye kiti kilicho juu ya Mungu (Isaya 14:13-14; Ezekieli 28:15; 1 Timotheo 3:6). Kiburi cha Shetani kilimfanya aanguke. Kumbuka usemi wa wengi “nita” katika Isaya 14:12-15. Kwa sababu ya dhambi zake, Mungu alimfukuza Shetani kutoka mbinguni.

Shetani akawa kiongozi wa ulimwengu na mfalme wa anga (Yohana 12:31; 1 Wathesalonike 3:5), na mwongo (Mwanzo 3; 2 Wakorintho 4:4; Ufunuo Wa Yohana 20:3). Jina lake linamaanisha Mwenye “majanga” au “mpingamizi.” Majina yake mengine ni, Ibilisi kumaanisha “mdanganyaji.”

Hata kama alifukuzwa kutoka mbinguni, bado anazidi kuinua kiti chake juu ya Mungu. Anayageuza yale Mungu anayafanya, akitumaini kuabudiwa na ulimwengu na anatia tumaini kwa pingamizi zote za ufalme wa Mungu. Shetani ndiye ako nyuma ya dini zote za uongo na dini za dunia. Shetani atafanya na kila kitu katika uwezo wake ili ampinge Mungu na wale wote wanaomfuata. Ingawa hatima ya Shetani imewekwa muhuri kuwa tanuru la moto milele (Ufunuo Wa Yohana 20:10).


Dk Syaga James